Amato wa Sion

Amato wa Sion (pia: Amat, Amé, Aimé; alifariki Breuil-sur-le-Lys, karibu na Amiens, Ufaransa, 690 hivi) alikuwa mmonaki Mkolumbani, halafu askofu wa mji huo, leo nchini Uswisi kuanzia mwaka 669, lakini baada ya miaka 5 ya uongozi bora alipelekwa uhamishoni na mfalme Theodoriki III[1] akafariki huko [2].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 13 Septemba[3].

  1. Butler, Alban. “Saint Amatus, Bishop and Confessor”. Lives of the Fathers, Martyrs, and Principal Saints, 1866. CatholicSaints.Info. 13 September 2013
  2. http://www.santiebeati.it/dettaglio/70200
  3. Martyrologium Romanum

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search